TANGAZO
MAJANGA! Mwanamke aliyejitambulisha kuwa ni mke wa ndoa wa jamaa aliyemtaja kwa jina la Ally Msangi, Rosita Yashira ameibuka na madai mazito kuwa staa wa filamu za Kibongo, Aisha Bui eti amezaa na mumewe huyo.
Anayelalamika kuibiwa mume.
Akizungumza kwa njia ya mtandao wa kijamii wa WhatsApp akiwa nchini Peru barani Asia, mwanamke huyo alisema kwamba Aisha amemwibia mumewe huyo ambaye amemtelekeza na watoto wawili na hatoi matumizi.
Alidai kwamba, alifunga ndoa na Msangi, mwenye uraia wa nchi mbili, Tanzania na Peru, mwaka 2007 ambapo wamejaliwa watoto wawili lakini mumewe alibadilika na kuwa na uhusiano na Aisha hadi akaamua kuhamia Tanzania na kuzaa naye.
“Mbaya zaidi Aisha amekuwa akinitumia picha akiwa na mume wangu, akinidhihaki kwamba niwaache wale bata.
“Inauma sana kwa sababu ni miezi saba sasa mume wangu hajui tunaishije na watoto na uwezo anao lakini hatumi matumizi yoyote, ukweli nateseka mno, kwa sasa mtoto mmoja anaumwa, sina fedha za kumtibu.
“Inauma sana kwa sababu ni miezi saba sasa mume wangu hajui tunaishije na watoto na uwezo anao lakini hatumi matumizi yoyote, ukweli nateseka mno, kwa sasa mtoto mmoja anaumwa, sina fedha za kumtibu.
“Nchi yangu iko kwenye hatari kila siku milio ya bunduki inasikika, hatuwezi kwenda nje kutafuta mahitaji na hata watoto wanacheza ndani, Aisha kaniharibia maisha,” alisema mwanamke huyo.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by Harocq
Post a Comment